ABOUT US









Msomaji Mpendwa
Assalaam alaykum

http://tibasahihi.blogspot.com/  ni mtandao ulioanzishwa kwa lengo la kuwaeleza wasomaji wake juu ya madhara ya ushirikina ili waachane naona badala yake waelekee kutafuta suluhisho la matatizo yao kwa kutumia namna ambayo Allaah ameielekeza kupitia kwa Mtume wake Muhammad S.A.W ni namna ambayo haina madhara yoyote kwa jamii kinyume na ilivyo kwa ushirikina kwani una madhara mengi sana na miongoni mwa madhara yake ni watu kutembea na mama,watoto ama dada zao eti ili wapate utajiri na huku wengine wakiuwa ndugu zao ama kuwafanya mandondocha,misukule na kadhalika.

Wakati huku katika tibasahihi hakuna uzito wa namna yoyote hakuna kubeba kitu wala nini kila kitu ni wepesi tu
Mwandishi wa mtandao huu ameshiriki kwa kipindi  cha zaidi ya miaka mitano katika kuwalingania kupitia kuwasomea na kuwaelekeza visomo mbalimbali vya tibasahihi watu kutoka mataifa mbalimbali na Alhamdulillah neema/rehma ya Allaah imepatikana.

Pia katika mtandao huu tutajitahidi tuwe tunawaletea wasomaji wetu Masomo mbalimbali yahusuyo namna ya kutekeleza ibada kama vile Swala, Zaka,Swaumu,Hijja, Kutendea wema majirani N.k
Lakini pia kwa kutumia rejea mbalimbali za uislam tutakuwa tukihimizana na kuhamasishana juu ya kuilinda na kuitetea amani ya nchi yetu na ushirikiano baina tunafanya yote kwa ajili ya kutafuta radhi ya Allah na tunamuomba Allah ajaalie juhudi hizi ziwemo katika mizani ya mema yetu siku ya kiama.

Lakini tunawaomba wasomaji wetu mtupatie ushirikiano wenu katika kuiwezesha juhudi hii ifikie malengo yake na ikitokea kuna makosa yawe ya uchapaji au uelewa tunaomba mtusahihishe maana wanaosoma mtandao wetu ni bora na wana elimu zaidi ya sisi tunaomiliki na kuandika humu hivyo tunashauri chochote chenye kulenga kufanikisha tulichokusudia kwa kutumia namba 0783698787 karibu nawe tushirikiane.