SHETANI ANASILIMU NA KUMTAPISHA UCHAWI MGONJWA BAADA YA KUSOMEWA RUQYAH

Ndugu Msomaji
Assalaamu alaykum,

Awali ya yote hatuna budi kumshukuru Mwenyezi Mungu Muumba Wa Mbingu Na ardhi na vilivyomo ndani yake na baina yake kwa kuuweze kukutana tena hapa kwenye mtandao wetu tunaoutumia kuelimishana mambo mbalimbali yanayotuwezesha kufahamu namna halali za kujitibu/kutibiwa bila ya kushiriki katika tiba za kishirikina.

Pia tunaomba mchango wako ili utuwezeshe kutoa kitabu cha dua za tiba na kinga ambacho kimesheheni shuhuda na mawaidha mbalimbali ni kitabu kitakachowasaidia, kuwaelimisha watu wengi zaidi, Toa sadaka yako sasa na wewe uingie katika watakaopata thawabu za watakaoongoka kutoka katika ushirikina na maovu mbalimbali, gharama za uchapaji wa kitabu ni kubwa hivyo msaada wako ni muhimu tuchangie kwa njia zifuatazo:-
 TIGO PESA No. 0715604488 M-PESA No. 0758293138 

kwa wale wasomaji wetu wa nje ya nchi wawasiliane nami kwa simu na whatsapp namba +255715604488
Leo nimeona niwafafanulie wasomaji wangu mambo machache kuhusu mashetani (mapepo) kwani watu wengi wamekuwa na uelewa mdogo kuhusu viumbe hawa.

Ukweli ni kwamba majini ni viumbe miongoni mwa viumbe wa mwenyezimungu kama Qur'aan inavyotueleza

وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ
"sikuumba majini na watu illa waniabudu" Adhariayaati:56

hapo tunapata ushahidi kuwa majini na wanaadamu wameumbwa na Allaah kwa ajili ya ...ibada tu. na sio kuwafanya wanadamu kuwa viti vyao maana mara nyingi binadamu mwenye shetani huitwa kiti, hupelekeshwa na shetani huyo kwa mambo mbalimbali.

na baada ya kuasi majini na wanaadamu ndio wakaitwa mashetani lakini maarufu kwa jina hilo la mashetani ni majini.
pia ni vyema tukatambua kuwa wapo majini wema kama walivyokuwepo wanaadamu wema na pia wapo majini waovu mfano wa wanaadamu vilevile.

Itambulike kuwa wapo majini waislamu,wakristo tena walokole, mayahudi,pia wapo wanaojitambulisha kwa makabila mbalimbali
nimepata kumlingania jinni wa kilokole na nilimtambua baada ya kupanda kichwani kwa mgonjwa na kuanza kunikemea kama wafanyavyo walokole,



Hii ilikuwa mwaka 2010 nilifuatwa na mmoja wa majirani zangu na kunishitakia tatizo la binti yake aliyekuwa anashindwa kwenda shule kwa sababu ya mashetani wakati huo akiwa kidato cha nne!

Siku ya kwanza nilipoelezwa matatizo ya binti huyo ilikuwa alhamisi sikumbuki tarehe lakini ilikuwa mwezi april,niliishia kuyasomea maji kisomo cha Ruqyah kisha nikawaaga na kuondoka kwakuwa nilikuwa nahitajika kwa mgonjwa mwengine aliyekuwa na hali ngumu zaidi kwa muda huo.

Nyuma yangu kumbe kulitokea matatizo mazito kiasi cha kusababisha mgonjwa kufungwa mikono na miguu niliyafahamu haya baada ya kurudi siku ya pili baada ya swala ya ijumaa,

Siku hiyo wakachukua namba zangu za simu lipofika saa 11:30 jioni wakanipigia simu kuwa hali ni mbaya kwakuwa sikuwa mbali na kwao nikarudi na kumkuta mgonjwa hana fahamu.

Nikaanza kumsomea kisomo cha Ruqyah baada ya muda shetani akapanda nikamlingania kuachana na dhulma alidai hana dini nikamlingania juu ya uislamu akanielewa ALHAMDU LILLAAH akasilimu na akaondoka, mara akapanda mwingine wa kike akaanza kufanya dhihaka mbalimbali lakini kwa kuwa nimejaaliwa kufahamu sehemu ya vitimbi vyao sikujali nilipoendelea na kisomo akaanza vituko vyake akiniambia ushindwe katika jina la yesu nami nikamuambia utashindwa wewe katika jina la ALLAH.

Ilinichukua muda mrefu wa kisomo ndipo kibao kilipombadilikia na kuanza majuto akimtaja yesu kwamba amemdanganya! nikamwambia sio kweli nikamueleza ukweli aliokuja nao yesu na jinsi ulivyopindishwa!

Kumbe Kabla Alikuwa Muislam!

Kumbe aliwahi kuwa muislamu akadanganywa na shetani mkristo akartadi,kwakuwa yule mgonjwa alikuwa akilalamikia maumivu ya kifua nilimuamuru yule shetani autoe uchawi wake akasema atakuja kuutoa mumewe (shetani wa kiume)kwani ndiye aliye uweka.
nikamlimngania uislamu akaukubali LILLAHIL HAMDU na yeye akasilimu,muda wa swala ya maghribi ulikuwa umeshafika tukaenda kuswali,

Tuliporudi nikaanza kusome dua kwa ajili ya kumuomba ALLAH alikinge eneo husika baada ya kuondoa picha zote za viumbe ahai ndani awali sikulizingatia hilo la kutoa mapicha kwa kuwa hali ya mgonjwa haikuwa nzuri nikafanya Ruqya katika  hali ya dharula ( lakini kuepusha mapicha,miziki n.k ni lazima kabla ya kisomo kwani malaika hawaingiii kwenye nyumba yenye picha za viumbe hai…)
kabla sijamaliza kusoma dua shetani akapanda kwa mgonjwa na kisomo kiliendelea kwa muda mrefu sana mwisho ALLAAH kaleta tawfiq yake kwani shetani alisalimu amri akakubali kuutoa uchawi aliomlisha mgonjwa na nilipomuhoji alimlisha wakati gani akasema wakati alipokuwa anakula chipsi shuleni (siku aliyoanguka mara ya kwanza)

Pia alilinganiwa uislam akasilimu na kutoka baada ya muda mfupi mgonjwa akarejewa na fahamu zake, nilipomuuliza mimi ni nani akanitaja jina langu na pia aliwatambua ndugu na wazazi wake,
nilipomuuliza kuhusu maumivu aliyokuwa anayalalamikia akajibu kuwa hayasikii tena! ALHAMDU LILLAAH kwani Munug ndie aliyeyatenda yote mimi nilikuwa ni sababu tu.

Jumatatu yule binti akaanza kwenda shule kama kawaida,Watu hawa Mwenyezi Mungu alitaka kuwaokoa na shirki kwani walishakwenda kwa mganga na kutakiwa kuku saba na mbuzi wawili,

KAMA UNAHITAJI KUSOMEWA DUA PIGA SIMU NAMBA +255715604488
NB:sina nia ya kuwakejeli watu kwa imani yao, kwani baadae inshaa ALLAH nitawaeleza pia kuhusu majini waislamu niliopata kuwalingania kwa wagonjwa na vituko vyao.



HUDUMA HII INAPATIKANA KWA WATU WOTE BILA KUBAGUA DINI YA MTU PIA TUNA HUDUMIA WANAOISHI NJE YA NCHI NA TANGU TUNAANZA TUMEKUWA TUKIWAHUDUMIA WATU WA ITIKADI ZOTE. NYOTE MNAKARIBISHWA.