QUR'AN YAMREJESHEA AJIRA BAADA YA KUFUKUZWA

Ndugu Msomaji 
Assalaamu alaykum
kwanza tumshukuru Mungu kwa kutupatia furasa nyingie kwa kuwa hai ktika muda huu na kuweza kuendelea na majukumu yetu ya kila siku.

Ni Matumaini yangu kuwa unaendelea vyema na majukumu yako ya kila siku nami nakuombea kheri na baraka katika harakati zako za utafutaji wa maisha.

Ndugu Msomaji leo nakuletea taarifa ya Dada anayeishi nchini Uingereza ambaye alinipigia simu Akaniambia kwamba namba yangu amepewa na Mmojawapo wa wasomaji wangu anayeishi nchini Sweden
Na kuniomba nimsaidie kufanya dua kwa ajili ya kumuomba Allah amrejeshe kazini kwake baada ya kufukuzwa kutokana na malalamiko aliyoyawasilisha kwa bosi wake kutokana na kutoridhishwa na tabia ya kutokuwa muadilifu (kupendelea) kwa bosi wake huyo.

Aliniambia kuwa alimua kuandika barua isiyokuwa na utambulisho wake na kuituma kwa Boss wake, lakini kwa bahati mbaya kutokana na uchunguzi uliofanyika akagundulika kuwa ni yeye ndie aliyeandika barua hiyo na hivyo akachukuliwa hatua ya kuondolewa kazini.

Akaniambia "mimi nilisema ukweli kwa Boss wangu nikimtaka awe muadilifu kwetu sote na ninaamini Mwenyezi Mungu anawapenda wasemao kweli na hiyo ndio kazi pekee niliyokuwa naitegemea kwa ajili ya kuendesha maisha yangu na pia kuwahudumia wanaonitegemea hivyo naomba unisaidie kuniombia dua na uniongoze kwenye dua ili Mwenyezi Mungu Anirejeshe kwenye kazi yangu niliyokuwa nikiifanya". 

Nami nililipokea ombi lake kama ilivyo desturi yangu nimeamua kuisaidia jamii kwa namna za halali kwa visomo/Dua mbalimbli kwa kutumia Qur'an na Sunnah nikampa utaratibu tuliodumu nao kwa muda  wa wiki chache hatimaye tukapata majibu yaliyotufurahisha sote.

وَمَن يَتَّقِ ٱللَّهَ يَجۡعَل لَّهُ ۥ مِنۡ أَمۡرِهِۦ يُسۡرً۬ا


Nakumbuka ni takribani miezi Mitano imepita tangu nipokee ombi hili na ALHAMDULILLAH ni miezi mitatu na nusu tangu Nilipopokea simu kutoka kwa msomaji wangu huyu akiwa na furaha kubwa akinifahamisha kuwa Allah amejibu maombi yetu na hatimaye amerudishwa kwenye kampuni ile ile na kitengo kile kile alichokuwa akifanya hapo mwanzo.

Hakika Allah ni muweza juu ya kila kitu namuomba Allah amsimamie mja wake na amfanyie wepesi kazi zake na aendelee kumkimbilia Allah katika kila linalomsibu maishani mwake.

Hata wewe unaweza kufanikiwa katika mambo yako iwapo utamtegemea Mungu katika Mambo yako yote na utawashinda maadui zako hata kama wakishirikiana kufanya dhulma.

Kwa yeyote mwenye tatizo na anahitaji Dua namab zangu ni +255715604488 
Lakini pia tuanendelea kupokea michango yenu kwa ajili ya
kuchapisha kitabu cha dua na kinga mbalimbali. 

Mwisho kabisa tunaunga mkono juhudi zote zinzofanya na serikali yetu ya Tanzania katika kuleta Maendeleo kwa wananchi wake, tunaendelea kuiombea serikali yetu mafanikio katika kututumikia.